Ayatullah Udhma Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amebainisha sifa na hila za kidanganyifu na kutokubali haki ubeberu wa dunia unaoongozwa na Marekani na kuongeza kuwa, njia pekee ya kuweza kumkatisha tamaa adui ni kusimama kidete na kuimarisha nguvu za taifa. Aliyasema hayo Jumatano asubuhi aliponana na makumi ya maelfu ya makamanda wa jeshi la Basiji na kusema kuwa, Basiji ni moja ya madhihirisho ya uthabiti, fakhari na utukufu wa mfumo wa utawala wa Kiislamu.
Habari ID: 1321100 Tarehe ya kuchapishwa : 2013/11/23